1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Misako na kamatakamata ya ufisadi yaendelea Ukraine

12 Novemba 2025

Uchunguzi wa madai ya ufisadi wa kampuni ya nyuklia ya Ukraine, Energoatom, unaendelea baada ya msako mkubwa uliofanywa na vyombo vya usalama kwenye nyumba ya waziri wa zamani wa nishati, German Galushchenko.

German Galushchenko
Waziri wa Sheria wa Ukraine, German Galushchenko, ambaye anachunguzwa sasa kwa ufisadi katika kampuni ya nyuklia ya nchi yake.Picha: Kenzo Tribouillard/AFP

Wizara ya sheria ya nchi hiyo iliyo kwenye vita na Urusi, ambayo kwa sasa inaongozwa na  Galushchenko imethibitisha kufanyika uchunguzi huo, na kwamba mwanasiasa huyo amekubali kutoa ushirikiano kwa mamlaka za upelelezi.

Baadaye, Ofisi ya Kupambana na Ufisadi ya Ukraine (NABU) ilitowa notisi ya tuhuma dhidi ya naibu waziri mkuu wa zamani, Oleksiy Chernyshov, ambaye amekuwa akichunguzwa tangu mwezi Juni kwenye kesi nyengine inayohusiana na sekta ya ujenzi.

Mwendesha mashtaka mkuu wa serikali, Serhiy Savytsky, amethibitisha notisi hiyo.

Licha ya kukabiliwa na uvamizi wa Urusi kwa miaka minne sasa, serikali ya Ukraine inayoongozwa na Rais Volodymyr Zelensky imekuwa ikishutumiwa kwa kuendekeza ufisadi. 

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW