Mjerumani aliuliwa kwa kupigwa risasi sita.
3 Agosti 2007Matangazo
Mjerumani huyo aliekuwa na umri wa miaka 44 alitekwa nyara mwezi jana pamoja na mjerumani mwingine katika jimbo la kati la Afghanistan Maidan Wardak.Uchunguzi uliofanywa na madaktari umeonesha kwamba mtu huyo alipigwa risasi kichwani.
Lakini msemaji wa wizara ya mambo ya nje bwana Martin Jäger ameeleza kuwa uchunguzi umeonesha kwamba mjerumani huyo ambae pia alikuwa mhandisi alizirai kabla ya kupigwa risasi sita.
Wakati huo huo serikali ya Ujerumani imeimarisha juhudi ili kuokoa maisha ya mjerumani mwengine ambae bado yumo katika mikono ya wateka nyara nchini Afghanistan.
Waziri wa mambo ya nje wa Ujerumani bwana Frank - Walter Steinmeier amesema juhudi zote sasa zitaelekezwa katika kumkomboa mjerumani huyo.
AM.