Mkutano kuhusu Mlango-Bahari wa Hormuz kufanyika London
22 Aprili 2026
Matangazo
Mkutano huo utakaoongozwa na Uingereza na Ufaransa, unalenga kuandaa mikakati madhubuti wa kulinda meli za mafuta, kama walivyojadili wiki iliyopita mjini Paris, Waziri Mkuu wa Uingereza Keir Starmer na Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron.
Mazungumzo hayo yatakayofanyika huko Northwood kaskazini mwa jiji la London yatazingatia uwezo wa kijeshi, masuala ya amri na udhibiti, kutegua mabomu ya ardhini na jinsi vikosi vya kijeshi vinavyoweza kupelekwa katika eneo hilo la Mlango-Habari wa Hormuz.