1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Merz ataka Ujerumani isimame imara kimataifa

20 Februari 2026

Kansela wa Ujerumani Friedrich Merz ameuambia mkutano mkuu wa chama chake cha CDU,kwamba Ujerumani inabidi isimame imara kuwa na sauti kubwa kimataifa katika wakati ulimwengu unakabiliwa na migogoro

Kansela  Friedrich Merz ameapa kutoruhusu AfD kuiharibu Ujerumani
Kansela Friedrich Merz ameapa kutoruhusu AfD kuiharibu UjerumaniPicha: Thilo Schmuelgen/REUTERS

Ujerumani inapaswa kusimama imara na kuchukuwa dhima kubwa zaidi katika jukwaa la dunia. Huo ni msimamo alioutowa Kansela Friedrich Merz kwenye mkutano mkuu wa chama chake cha CDU uliofunguliwa hivi leo mjini Stuttgart. Merz anatarajiwa kuwania tena nafasi ya mwenyekiti wa chama hicho kwenye mkutano huo.

Mkutano mkuu wa chama cha  Christian Democratic Union, CDU wa siku mbili unafanyika wakati  ulimwengu ukishuhudia hali ya wasiwasi unaosababishwa na migogoro. 

Kansela Friedrich Merz amewaambia wanachama wa chama chake kwamba utaratibu wa kidunia uliokuwa ukizingatia sheria za kimataifa haupo tena na kwahivyo Ujerumani inapaswa kusimama imara kujiweka mbele kimataifa na kuweka mikakati mipya katika Ulaya iliyo na mshikamano.

''Ulimwengu unapitia kipindi cha kujipanga upya. Ulaya inakabiliwa na shinikizo na Ujerumani inahitajika zaidi kuliko wakati mwengine wowote. Tunakabiliwa na changamoto kubwa. Tunataka kujiimarisha kiuchumi,tunataka kuilinda nchi yetu na kuifanya kuwa na nguvu zaidi za kijeshi. Tunataka kuendeleza ustawi endelevu wa taifa na tunahitaji kuimarisha sekta ya uvumbuzi kadhalika tunataka kuurudisha mshikamano wetu wa kijamii.''

Hotuba yake mjini Stuttgart kansela Merz imegusia masuala mbali mbali ya ndani ya nchi na ya kimataifa akikumbusha kwamba Marekani itabakia kuwa mshirika wa Ujerumani licha ya kuweko mivutano ya kisiasa na nchi hiyo.

Lakini katika siasa za ndani ameapa kutotowa mwanya kwa  chama cha  siasa kali za mrengo wa kulia cha AfD kuiharibu Ujerumani.

Angela Merkel na Armin Laschet kwenye mkutano mkuu wa chama cha CDU Picha: Frank Hoermann/SvenSimon/picture alliance

Kwa mara ya kwanza tangu mwaka 2021 alipondoka madarakani Kansela wa zamani Angela Merkel ameshiriki mkutano huo  wa chama cha CDU akikaribishwa kwa makofi mengi na wanachama.Kansela Merz katika mtihani: jinsi anavyoshughulikia mgogoro wa serikali

Mara ya mwisho binafsi Merkel kushiriki mkutano huo ni mwaka 2019. Wamehudhuria pia viongozi wengine wa zamani wa chama hicho Annegret Kramp-Karrenbauer na Armin Laschet.

Pamoja na mengine mkutano huo unatarajiwa kumchaguwa mwenyekiti wake mpya ambapo Kansela Merz anatafuta uungwaji mkono wa kurejea kukiongoza chama hicho.Wabunge vijana wa Ujerumani watikisa siasa

Mkutano huo unafuatiliwa kwa karibu nchini Ujerumani na hasa kuona ni kwa kiasi  gani Merz atakafanikiwa kuungwa mkono.

Mkutano huo wa siku mbili umekuja wakati ukiwa ni mwanzo wa mwaka wa hekaheka za uchaguzi  kwa chama hicho cha CDU  huku majimbo matano yakitarajia kufanya chaguzi zake ikiwa ni pamoja na jimbo la Baden- Wurttemberg litakaloanza uchaguzi mwanzoni mwa mwezi Machi.

 

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW