1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Mkutano wa kilele wa AU waendelea nchini Ethiopia

15 Februari 2026

Mwenyekiti wa Tume ya Umoja wa Afrika Mahamoud Ali Youssouf amesema kutoka Sudan hadi Sahel, mashariki mwa Kongo, Somalia na kwingineko, watu wa bara la Afrika wanaendelea kulipia gharama ya ukosefu wa utulivu.

Ethiopia Addis Ababa 2026 | Umoja wa Mataifa
Kikao cha Umoja wa Mataifa mjini Addis Ababa, Ethiopia mnamo 14, Februari 2026Picha: Eskinder Firew/DW

Youssouf ametoa wito wa kusitishwa mara moja kwa kile alichokiita "maangamizi ya watu wa Palestina, kauli iliyomfanya waziri mkuu wa Palestina Mohammad Mustafa, kuishukuru Afrika kwa mshikamano wake.

Youssouf amesema hayo wakati wa mkutano wa 39 wa Umoja huo  wa Afrika uliofunguliwa jana mjini Addis Ababa nchini Ethiopia utakaodumu kwa siku mbili.

Mkutano huo wenye kauli mbiu ''maji na usafi wa mazingira'', utajadili mustakabali wa bara hilo lenye idadi ya watu bilioni 1.4.

Mazungumzo yatajumuisha hatua za bara hilo za kupambana na mabadiliko ya tabia nchi na majanga ya kibinadamu kufuatia kupunguzwa kwa misaada kutoka kwa washirika wa kimataifa kama vile Marekani.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW