1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Mkutano wa kilele wa mataifa ya BRICS waanza Afrika Kusini

22 Agosti 2023

Viongozi wa nchi zinazoinukia kiuchumi za kundi la BRICS wanakutana nchini Afrika Kusini kuanzia leo Jumanne hadi Alhamis.

Südafrika BRICS-Gipfel in Johannesburg
Picha: Sergei Bobylev/dpa/TASS/picture alliance

Mataifa wanachama wa BRICS ambayo ni Brazil, Urusi, India, China na Afrika Kusini, yanawakilisha robo ya uchumi wa dunia. Nchi kadhaa zimeonesha nia ya kutaka kujiunga na kundi hilo.

Rais wa Afrika Kusini Cyril Ramaphosa amewakaribisha Rais wa China Xi Jinping, Waziri Mkuu wa India Narendra Modi, Rais wa Brazil Luiz Inacio Lula da Silva na baadhi ya viongozi wengine 50. Rais Ramaphosa ameserma Afrika kusini na China zina msimamo mmoja kuhusu swala la kuongeza wanachama wapya.


"Afrika Kusini na China zina maoni sawa kuhusiana na kuongeza wanachama kwenye kundi la BRICS na tunaazimia kufanya majadiliano na viongozi wengine wa BRICS baadaye leo kwenye mkutano wetu."

Mkutano wa kilele wa nchi za BRICS waanza rasmi Johannesburg


Wakati huo huo rais wa Afrika Kusini amesema amejadili juu ya mzozo kati ya Urusi na Ukraine na rais wa China Xi Jinping, katika mazungumzo yao kabla ya mkutano wa BRICS mjini Pretoria.

Kwa upande wake rais wa China Xi Jinping amesema mkutano kati yake na rais wa Afrika Kusini ulikuwa ni wenye tija na kwamba wamebadilishana maoni kuhusu maswala mbalimbali na wamefikia makubaliano muhimu.