1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaUkraine

Mkutano wa kimataifa wa amani Ukraine wafungua Uswisi

15 Juni 2024

Mkutano wa kimataifa wa kujadili amani nchini Ukraine umefunguliwa Jumamosi katika eneo la mapumziko la Bürgenstock nchini Uswisi. Urusi hata hivyo haijaalikwa kwenye mkutano huo.

Mkutano wa amani ya Ukraine nchini Uswisi
Viongozi kadhaa wa Ulaya wanahudhuria pia, wakiwemo Rais wa Ufaransa Macron, na Kansela wa Ujerumani Scholz.Picha: Michael Buholzer/dpa/picture alliance

Viongozi wa kitaifa na wawakilishi wengine wa ngazi za juu kutoka mataifa 92 na mashirika ya kimataifa wanatarajiwa kuhudhuria mkutano huo, kujadili masuala kuanzia usafirishaji wa nafaka kutoka Ukraine, usalama wa mtambo wa nyuklia wa Zaporizhzhya unaokaliwa na vikosi vya Urusi na masuala ya kitu, ikiwemo kubadilishana wafungwa.

Urusi hata hivyo haijaalikwa kwenye mkutano huo. Marekani ambayo ndiyo mshirika muhimu zaidi wa Ukraine, inawakilishw ana makamu wa Rais Kamala Harris. Viongozi kadhaa wa Ulaya wanahudhuria pia, wakiwemo Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron, na Kansela wa Ujerumani Olaf Scholz.

Urusi kwa sasa inakalia karibu humusi moja ya ardhi ya Ukraine, ikiwemo Rasi ya Crimea iliyoinyakua mwaka 2014. Rais Vladmir Putin aliitaka Ukraine kukabidhi maeneo ya Donetsk, Luhansk, Kherson, Zaporizhzhya na rasi ya Crimea kama sharti la kukomesha vita, masharti ambayo Kyiv imeyataja kuwa ya kipuuzi.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW