1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Mkutano wa matayarisho wa kuunda serikali ya mseto Ujerumani

Sekione Kitojo
4 Januari 2018

Wahariri wa magazeti nchini Ujerumani wamejishughulisha na masuala ya mkutano wa matayarisho wa kuunda serikali ya mseto kati ya  CDU/CSU na SPD, uchunguzi juu ya sababu zinazopelekea wakimbizi kujihusisha na uhalifu.

Deutschland Ende Jamaika-Koalition Sondierungsgespräche | Angela Merkel; Bundeskanzlerin
Picha: Reuters/A. Schmidt

 

 

Tuanze  na  gazeti  la  Rhine-Necker  Zeitung la  mjini  Heidelberg , mhariri  anazungumzia mkutano  wa  matayarisho  ya  kikao cha mazungumzo ya kuunda  serikali  ya  mseto  nchini  Ujerumani kufuatia  uchaguzi wa  mwezi  Septemba  mwaka  jana. Mhariri anaandika:

Ujerumani  bado  haina  serikali rasmi  hadi sasa  na  kama alivyosema  kiongozi  wa  chama  ndugu  na  chama  tawala cha CDU , Horst Seehofer wa chama  cha  CSU kwamba  hadi itakapofika  wakati  wa  sikukuu  ya  pasaka serikali  itakuwa imekwisha  kamilika. Lakini  hilo  bado  liko  mbali  sana. Hata kama  kabla  ya  mkutano  huu  wa  matayarisho, hali  ya kuaminiana  iliongezeka, maudhui  juu  ya  mazungumzo  hayo bado hayajapata  muafaka. Kwa mfano  suala  la kubana sera za uhamiaji ambazo chama  cha  CSU kimewasilisha  kama mapendekezo  yake, hazipendelewi  na  chama  cha  SPD. Kumekuwa  pia  na hali  ndogo  ya  kuwapo makubaliano kuhusu  mageuzi katika bima  ya  afya.  Merkel  na  Seehoffer wanapaswa  kuridhia  mengi zaidi  iwapo  wanataka  serikali imara.

Gazeti  la  Reutlinger General-Anzeiger linazungumzia  utafiti  kuhusu sababu  zinazopelekea  wakimbizi  kujihusisha  na  matukio  ya uhalifu hapa  nchini  Ujerumani. Gazeti  linaandika.

Hadi  sasa haileti  maana , kuwaweka  wakimbizi  wote  katika kapu  moja. Pamoja  na  hayo  mtu  hapaswi  kufumbia  macho matukio  ya  wakimbizi. Ujerumani  inapaswa  kufungua milango  yake  kwa  wakimbizi  wanaotoka  katika  mataifa yenye  vita, lakini  wale  wakimbizi  wanaokimbia  nchi  zao kutokana  tu  na  umasikini  ama   wakimbizi  wa  kiuchumi hawapaswi  kupewa  matumaini  ya  kuishi hapa. kitu kinachosikitisha  ni  kwamba  baadhi  yao  hujiingiza  katika matendo  ya  kihalifu. Unaonesha utafiti. Kutokana  na  hilo  ni sheria  za  uhamiaji  zilizo  wazi  pekee  ambazo  zinaweza kuzuwia  hali  hiyo. Ukweli  lakini  ni  kwamba, taifa  na  jamii wanapaswa  kufanya zaidi kwa wakimbizi  ambao  hawana nafasi  ya  kubakia  warejeshwe  makwao. Hii  sio chuki  dhidi ya  watu  kutoka  nje, lakini  ni  ishara ya  kujilinda kidemokrasia.

Nalo  gazeti  la  Hannoversche Allgemeine  , likizungumzia  mada hiyo  linaandika:

Itabidi  kutafuta  haraka  kampuni  itakayowashughulikia wakimbizi. ambayo  inaweka  wazi  kwamba  , yeyote atakayefuata  sheria anaweza  hata  akaileta  familia  yake. Kwa yule  ambaye atafuata  sheria , na  hii  itaanzia  kwa  yule ambaye  hajatoa utambulisho  wa  uongo,  atapewa  fedha mara  mbili  zaidi, na  hatojihusisha  na  udhalilishaji  wa wanawake  ama  matukio  ya  kihalifu. Wale  wataoapatikana  na hatia  kama  hizo  haraka  watarejeshwa  makwao. Hii itawafanya  wakimbizi  vijana  kufuata  sheria  na  kuwatuliza. Yule atakayefuata  sheria  atapewa  fursa .

Kuhusu  maandamano  yaliyotokea  nchini  Iran gazeti  la  Märkische Oderzeitung  la  mjini  Frankfurt  linaandika.

Tofauti  na  mwaka  2009  vijana  wa  tabaka  la  kati hawakupambana  mara  hii  katika  miji  mikubwa  kuhusu udanganyifu  katika  uchaguzi, na  waandamanaji  hawakuwa na  uongozi  wa  kisiasa. Pamoja  na  hayo  mapambano  dhidi ya  watawala  yanaendelea  kubaki  bila  mwelekeo , na  hali inaendelea  kuwa  vile  vile  ambapo watawala  bado hawajaweza  kuwasikiliza raia  wao. Mbali  ya  hivyo , bajeti  ya taifa  inapaswa kugawanywa  kwa  usawa, ili  iwafikie wote na kupunguza  mzigo wa  wakimbizi  kutoka  Iran  kwenda  katika mataifa  jirani  ya  Kiarabu.

 

Mwandishi: Sekione Kitojo / inlandspresse

Mhariri: Gakuba, Daniel