1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Mkutano wa Usalama wa Munich 2026 wahitimishwa Jumapili

16 Februari 2026

Mkutano wa Usalama wa Munich wa mwaka huu wa 2026, umemalizika Jumapili baada ya siku tatu za mijadala kuhusu migogoro inayoshuhudiwa kote ulimwenguni ikiwa ni pamoja na vita vya Ukraine na mzozo wa Mashariki ya Kati.

Bendera ya Mkutano wa Usalama wa Munich wa mwaka huu wa 2026
Bendera ya Mkutano wa Usalama wa Munich wa mwaka huu wa 2026Picha: Frank Hoermann/SvenSimon/picture alliance

Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani Marco Rubio amesema Marekani  haina nia ya kuifanya Ulaya kuwa "kibaraka" , lakini mshirika ambaye atakuwa tayari kuunga mkono maono ya Rais Donald Trump ya "kufufua" utaratibu wa kimataifa.

Hata hivyo, mkutano huo wa Munich ulishuhudia ukosoaji hasa kuhusu nafasi na ushiriki mdogo wa bara la Afrika, hasa kutokana na kuwa mijadala katika mkutano huo haikuangazia kwa kina migogoro inayoikumba Afrika kama vile Sudan, mashariki mwa DRC, au katika kanda ya Sahel.

 

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW