1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaUganda

Mkuu wa jeshi la Uganda amtishia kifo kiongozi wa upinzani

21 Januari 2026

Mkuu wa jeshi la Uganda, ambaye pia ni mtoto wa Rais Yoweri Museveni, ametishia kumsaka na kumuua kiongozi wa upinzani, Bobi Wine, ambaye yuko mafichoni baada ya kukimbia uvamizi nyumbani kwake.

Uganda Kampala 2026 | Bobi Wine
Kiongozi wa upinzani wa Uganda, Bobi Wine, ambaye ametishiwa kuuawa na mkuu wa majeshi, Jenerali Muhoozi Kainerugaba.Picha: Rian Cope/AFP/Getty Images

Jenerali Muhoozi Kainerugaba aliandika kwenye mtandao wa X siku ya Jumanne (Januari 20) kwamba walikuwa wamewauwa wale aliowaita magaidi 22 wa chama cha NUP (cha Bobi Wine) na kwamba anatazamia "wa 23 atakuwa Kabobi!"

Kiongozi huyo wa upinzani, ambaye aliwania urais kupingana na Museveni, alitangazwa na tume ya uchaguzi kushindwa na Museveni, na tangu Jumamosi amekuwa mafichoni baada ya kuvishutumu vikosi vya usalama kutaka kumteka.

Kainerugaba alimpa Wine masaa 48 ya kujisalimisha ama akabiliwe na hatua kama muasi.

Mwenyewe Wine aliandika kwenye mitandao ya kijamii kulitaka jeshi kuondoka kwenye nyumba yake, ambako alisema familia yake haikuwa salama.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW