1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaUkraine

Katibu Mkuu wa NATO Jens Stoltenberg aizuru Ukraine

20 Aprili 2023

Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Kujihami ya NATO Jens Stoltenberg anazuru Ukraine kwa mara ya kwanza tangu Urusi ilipoanza uvamizi kamili nchini humo zaidi ya mwaka mmoja uliopita. NATO haina uwepo wake rasmi nchini Ukraine.

Ukraine | Jens Stoltenberg in Kiew
Picha: Alina Yarysh/REUTERS

Kama shirika la nchi 31 wanachama, NATO hutoa tu msaada usio wa silaha kwa serikali ya Ukraine kama vile jenereta, vifaa vya matibabu, mahema, sare za kijeshi na bidhaa nyingine. Stoltenberg alikuwa Kyiv kabla ya vita, lakini hii ndio ziara yake ya kwanza wakati huu wa vita na inasisitiza ahadi za muda mrefu za jumuiya hiyo katika ulinzi wa uhuru wa Ukraine.

Wakati huo huo, mkuu wa majeshi ya Ukraine amesema Urusi imefanya mashambulizi zaidi ya 20 ya ndege za rubani zisizoruka na rubani zilizotengenezwa Iran, katika saa 24 zilizopita. Amesema mifumo ya ulinzi ya Ukraine iliweza kuzidungua droni 21 kati ya 26 ambazo zimetengenezwa kuruka hadi sehemu inayolengwa na kisha kulipuka.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW