Golikipa wa Ujerumani Manuel Neuer atangaza kustaafu
30 Juni 2026
Golikipa mkongwe wa Ujerumani Manuel Neuer ametangaza kustaafu kuitumikia timu ya taifa ya Ujerumani mara tu baada ya kutolewa na Paraguay katika mchezo wa raundi ya 32 katika michuano ya Kombe la Dunia.
Alipoulizwa na waandishi wa shirika la habari la Ujerumani la ARD, Neuer amesema huo ndio ulikuwa mchezo wake wa mwisho akiwa na jezi ya timu ya taifa ya Ujerumani.
Hata hivyo, awali mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 40 alishatangaza kustaafu kuichezea timu hiyo ya taifa kabla ya kurejeeshwa tena na kocha Julian Nagelsmann.kuondolewa mapema kwa Ujerumani: Tatizo ni nini?
Manuel Neuer alikuwa sehemu ya kikosi cha Ujerumani kilichobeba ubingwa wa Kombe la Dunia mwaka 2014 nchini Brazil na anamaliza muda wake akiwa na rekodi ya kipa aliyecheza mechi nyingi zaidi duniani.