1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaAsia

Mlipuko kwenye mgodi wa mawe nchini China wawauwa watu 90

23 Mei 2026

Mlipuko wa gesi kwenye mgodi wa makaa ya mawe katika jimbo la Shanxi kaskazini mwa China, umewauwa takriban watu 90. Haya yameripotiwa leo na vyombo vya habari vya serikali.

China Changzhi 2026 | Mlipuko wa mgodi wa mawe
Maafisa wa uokoaji katika mgodi wa mawe wa Liushenyu mnamo Mei 23, 2026Picha: Cao Yang/Xinhua/AP Photo/picture alliance

Shirika la habari la Xinhua limeripoti kuwa ajali hiyo katika mgodi wa Liushenyu ulioko katika jiji la Changzhi ilitokea jana jioni. Takriban wafanyikazi 247 walikuwa kazini wakati huo.

Xinhua pia imesema chanzo cha  mlipuko huo bado kinachunguzwa na juhudi za uokoaji zinaendelezwa. Wengi wa wafanyakazi hao walijeruhiwa na gesi yenye sumu. Haya ni kulingana na shirika la habari la serikali CCTV.

Xinhua imeripoti kuwa Rais wa nchi hiyo Xi Jinping ametoa wito wa juhudi za kila namna kufanyika kuwaokoa waliotoweka na kufanywa kwa uchunguzi wa chanzo cha ajali hiyo huku akitaka waliohusika kuwajibishwa.

Mkoa wa Shanxi unajulikana kama mkoa mkuu wa uchimbaji madini wa makaa ya mawe  nchini China.

 

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW