1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
JamiiIran

Mlipuko mkubwa waitikisa bandari nchini Iran na kujeruhi 516

26 Aprili 2025

Mlipuko mkubwa na moto umeitikisa bandari ya Shahid Rajaei kusini mwa Iran na kuwajeruhi takriban watu 516, hii ikiwa ni kulingana na televisheni ya taifa.

Iran Bandar Abbas 2025 | Mlipuko
Moshi mzito ukiwa umetanda kwenye eneo la Shahid Rajaee ambako mlipuko umetokea na kujeruhi watu wengiPicha: IRIBNEWS/AFP

Mlipuko huo ulitokea katika bandari hiyo iliyopo nje kidogo ya kituo kikuu cha usafirishaji wa makontena cha Bandar Abbas huko Iran kinachoshughulikia karibu tani milioni 80 za bidhaa kwa mwaka.

Televisheni ya taifa ya Iran imeripoti kwamba, watoa huduma ya kwanza walikuwa wakijaribu kufika eneo hilo na wengine wakijaribu kuzihamisha bidhaa. Chanzo cha moto huo bado hakijajulikana.