Mlipuko wa Ebola DRC: Visa 1003, vifo 254
23 Juni 2026
Matangazo
Hii ni takwimu mpya iliyotolewa jana na taasisi ya Kitaifa ya Afya ya Umma ya DRC (INSP) kufuatia mlipuko wa Ebola uliotangazwa Mei 15 mwaka huu.
Karibu visa vyote vya maambukizi vimeripotiwa katika jimbo la Ituri, Kivu Kaskazini na Kivu Kusini maeneo yanalokumbwa na migogoro ya makundi yenye silaha.
Virusi hivyo pia vimeenea hadi nchi jirani ya Uganda, ambapo Shirika la Afya Duniani WHO limerekodi visa 20 na vifo viwili, ingawa serikali mjini Kampala ilisema mapema mwezi huu kuwa ugonjwa umedhibitiwa. Mlipuko huu wa Ebola unaotokana na aina adimu ya virusi vya Bundibugyo ambayo haina chanjo au matibabu rasmi.