1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

MOGADISHU: Kituo cha polisi kimevamiwa Somalia

3 Agosti 2007

Si chini ya watu 10 wameuawa katika mashambulizi yaliyozuka mji mkuu wa Somalia,Mogadishu ikishukiwa kuwa yamefanywa na waasi wa makundi ya Kiislamu.Katika shambulio moja peke yake,watu wasiopungua 9 waliuaw,baada ya kituo cha polisi kuvamiwa wakati wa usiku,kaskazini mwa Mogadishu. Mpita njia mmoja pia aliuawa,baada ya mshambulizi kurusha gruneti kwenye mkahawa unaotumiwa sana na maafisa wa kijeshi,kusini mwa Mogadishu.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW