MOGADISHU: Kombora limeripuka karibu na kasri la rais
14 Machi 2007Matangazo
Kasri la rais katika mji mkuu wa Somalia, Mogadishu limeshambuliwa kwa makombora saa chache tu baada ya rais Abdullahi Yusuf kuhamia jengo hilo.Rais Yusuf,aliwasili Mogadishu siku moja baada ya bunge kukubali kuhamia tena mji mkuu kutoka ngome ya serikali mjini Baidoa.Maafisa wa serikali wamesema,watu 2 waliuawa katika shambulio hilo,lakini kwa mujibu wa mashahidi, idadi ni kubwa zaidi.Mapigano yameripotiwa pia katika maeneo mengine ya makazi mjini Mogadishu.