Atom Müll Seminar
8 Julai 2008Matangazo
Wanasayansi kutoka mataifa 14 barani Afrika na Ulaya wanakutana mjini Mombasa, Kenya, kutafuta mbinu za kuboresha usimamizi wa matumizi bora ya zana za atomiki na miunzi ya nuru shishi katika kanda ya Afrika Mashariki. Kongamano hilo, linalofadhiliwa na Shirika la Umoja wa Mataifa kuhusu Kawi ya Atomiki, linalenga kuyaleta pamoja mataifa ya bara la Afrika katika juhudi za kubuni mikakati ya kukabiliana na utupaji movyo wa malimbikizi au kuingizwa bidhaa zenye miunzi ya nusu shishi.
Mwandsihi wetu wa Mombasa, Eric Ponda, ametutumia ripoti ifuatayo: