Moscow
31 Januari 2005Moscow:
Rashia inaunga mkono hatua zilizochukuliwa na rais wa Palastina Mahmoud Abbas kukomesha mapambano kwa mtutu wa bunduki katika mashariki ya kati."hayo ni kwa mujibu wa taarifa ya pamoja kati ya Rashia na Palastina iliyotiwa saini na marais Vladimir Putin na Mahmoud Abbas hii leo huko Kremlin.Viongozi hao wawili wameelezea umuhimu wa kuanzishwa haraka mazungumzo kati ya Israel na Palastina na kufungua njia ya kushirikiana katika sekta ya usalama .Taarifa hiyo imeelezea pia umuhimu wa kutiwa njiani mpango wa pili wa amani ulioandaliwa na Marekani,rashia,Umoja wa mataifa na umoja wa ulaya.Wakati huo huo viongozi wa utawala wa ndani wa Palastina wamesema msichana wa miaka 10 ameuliwa hii leo na jeshi la Israel akiwa katika shule ya kambi ya wakimbizi ya Rafaa huko Gaza..