1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
Janga

Moto na milipuko kambi ya kijeshi Burundi vyaua watu 13

2 Aprili 2026

Watu 13 wamefariki na wengine 57 kujeruhiwa kufuatia mlipuko mkubwa uliosababishwa na moto katika kambi ya kijeshi nchini Burundi.

Burundi, Bujumbura 2026 | Milipuko na moshi mkubwa baada ya moto katika kambi ya kijeshi
Jeshi limesema milipuko hiyo ilisababishwa na hitilafu ya umeme na kwamba hali imedhibitiwa kikamilifuPicha: Ju Yinhe/Xinhua/IMAGO

Jeshi limesema moto huo ulizuka usiku katika ghala la kuhifadhia vifaa vya kijeshi na kusababisha milipuko kadhaa baada ya risasi na mabomu kulipuka.

Msemaji wa jeshi, Gaspard Baratuza, amesema chanzo cha moto huo ni hitilafu ya umeme, akisisitiza kuwa hakukuwa na shambulio lolote dhidi ya kambi hiyo.

Tukio hilo lilitokea katika eneo la Musaga, nje kidogo ya jiji la Bujumbura, ambapo wakazi walikimbia kwa hofu huku milipuko ikisikika kwa umbali mkubwa.

Maafisa wamewataka wananchi kutoa taarifa kuhusu mabaki ya milipuko ambayo hayajalipuka, wakati hali ikianza kurejea kawaida.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW