JangaPeru
Moto ulozuka mji mkuu wa Peru waendelea kuwaka
6 Machi 2025
Matangazo
Moto huo ulizuka siku ya Jumatatu kwenye bohari moja iliyokuwa ikiendeshwa bila vibali katika wilaya ya Barrios Altos. Idara ya Zimamoto imesema moto huo ulisambaa kutoka jengo hilo kwenda mengine ambapo tangu wakati huo majengo manne yameungua na kuporomoka.
Mkuu wa idara hiyo Carlos Malpica amesema kukosekana kwa miundombinu ya kusambaza maji kumeongeza wasiwasi kuwa moto huo utaendelea kuwaka kwa siku kadhaa zinazokuja.
Familia kadhaa zimehamishwa kutoka nyumba zinazowaka moto, huku watu wengi wakijaribu kuondoka na majokofu, viti na magodoro.
Hakuna majeruhi wala kifo kilichoripotiwa hadi sasa lakini kiongozi wa manispaa ulikotokea moto huo amesema familia nyingi zimepoteza mali.