1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Mpaka kati ya DRC na Burundi wafunguliwa

23 Februari 2026

Mpaka wa Kavimvira ulifungwa kufuatia operesheni ya kijeshi ya kundi la M23 linalosaidia na Rwanda kwenye eneo hilo

Operesheni ya waasi wa M23 ilisababisha mpaka kati ya Burundi na DRC kufungwa kwa miezi kadhaa
Operesheni ya waasi wa M23 ilisababisha mpaka kati ya Burundi na DRC kufungwa kwa miezi kadhaaPicha: AFP

Mpaka kati ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo na Burundi umefunguliwa tena hivi leo Jumatatu baada ya kufungwa kwa zaidi ya miezi miwili.

Taarifa hiyo imethibitishwa na maafisa wa Kongo na polisi wa Burundi ambao wamezungumza na shirika la habari la AFP.Maelfu ya Wakongo wakimbilia Burundi baada ya M23 kuudhibiti mji wa Uvira

Vyanzo vyote hivyo vimesema mpaka wa Kavimvira ambao unatumiwa zaidi kwa shughuli za kibiashara na ambao ulifungwa mwezi Desemba kufuatia operesheni ya kundi la waasi wa M23 wanaoungwa mkono na Rwanda, ulifunguliwa mapema leo asubuhi.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW