1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Msemaji wa Kijeshi wa M23 auuwa DRC

1 Machi 2026

Jeshi la M23, linalopigana mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, jana Jumamosi lilithibitisha kifo cha msemaji wake wa kijeshi, Willy Ngoma, aliyeuawa katika shambulio la droni la jeshi la Kongo.

DRC Kibumba 2022 | Msemaji wa kijeshi wa M23 Willy Ngoma
( Maktaba)Msemaji wa kijeshi wa M23 Willy Ngoma akiandamana na maasiwa wa KDF.Picha: Moses Sawasawa/AP Photo/picture alliance

Tangazo hilo limejiri siku chache baada ya majeshi ya serikali ya Kongo kulenga kundi hilo karibu na mji wa Rubaya, eneo muhimu la uchimbaji madini katika wilaya ya Masisi, mkoa wa Kivu Kaskazini.

Katika taarifa yake M23 iliyosainiwa na msemaji wake wa kiraia, Lawrence Kanyuka imesema utawala wa Kinshasa umekiuka makusudi usitishaji mapigano na kutangaza vita kamili” kwa kuzindua mashambulizi ya droni nyuma ya mstari wa mbele wa vita.

Willy Ngoma na maafisa wengine watano wa makundi ya waasi mashariki mwa DRC waliwekewa vikwazo na Umoja wa Mataifa, wakituhumiwa kupanga au kutekeleza ukiukaji wa haki za binadamu na sheria ya kimataifa ya kibinadamu.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW