1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Msemaji wa kundi la waasi la M23 auawa

24 Februari 2026

Msemaji wa kijeshi wa kundi la waasi wa M23, Willy Ngoma ameuawa mashariki mwa Kongo hii siku ya Jumanne.

DR Kongo Bukavu 2025 | Msemaji wa M23-Willy Ngoma na waajiriwa wapya | Uwanja wa Uhuru
Msemaji wa kundi la waasi wa M23 Willy Ngoma(katikati) auawa kwenye shambulizi la droniPicha: AFP

Shirika la habari la Reuters limeripoti taarifa hizo likinukuu vyanzo vitatu vya kijeshi ikiwemo afisa mmoja wa kundi la M23

Kulingana na vyanzo hivyo, Ngoma ameuawa katika shambulizi la droni lililotokea katika eneo la Rubaya jimboni Kivu Kaskazini.

Siku kadhaa zilizopita, Willy Ngoma alinusurika kuuawa katika mashambulizi kadhaa ya droni yaliyofanywa kwenye eneo hilo la vikosi vya jeshi la Kongo.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW