1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

MSF yalaani kuzuiwa kwa misaada ya kibinadamu Sudan Kusini

30 Januari 2026

Shirika la Madaktari Wasio na Mipaka (MSF) limelaani leo vikwazo vya upatikanaji wa misaada ya kibinadamu nchini Sudan Kusini huku mapigano yakiongezeka kati ya makundi hasimu katika kipindi cha mwezi mmoja uliopita.

Sudan Tawila 2025 | huduma za matibabu
Wakimbizi wanaougua wakipata matibabu katika hospitali ya muda inayoendeshwa na MSF katika eneo la Tawila nchini Sudan mnamo Novemba 3. 2025Picha: Mohamed Jamal/REUTERS

Limesema hilo ndilo shirika la pekee la huduma za afya nchini humo linalowahudumia takriban watu 400,000, na kuongeza kuwa serikali imezuia safari za ndege za kibinadamu kwenda maeneo ya Lankien, Pieri, na Akobo, na kwamba pia imewazuia kusambaza madawa na wafanyakazi na kuwahamisha wagonjwa mahututi.

Katika taarifa yake, MSF imesema maafisa wa timu yake huko Pieri, walilazimika kuhama kituo chake jana kutokana na hatari ya kutokea kwa vita.

Pia waliwahamisha wagonjwa na kuchukuwa vifaa vya dharura walipokuwa wakiukimbia mji huo wakiwa na wakaazi wa eneo hilo.

Mkuu wa MSF tawi la Sudan  Abdalla Hussein, amesema wagonjwa watakufa ikiwa serikali itaendelea kuzuia misaada ya kibinadamu na kupelekwa kwa huduma za matibabu Jonglei.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW