SiasaVenezuela
Machado "Nalenga mabadiliko ya amani baada ya Maduro"
12 Desemba 2025
Matangazo
Kiongozi huyo wa upinzani nchini Vanezuela aliwasili mjini Oslo mapema jana, akipuuzilia mbali zuio la muda mrefu la kusafiri alilowekea na mamlaka za Venezuela baada ya kujificha kwa zaidi ya mwaka mmoja.
Machado alipozungumza na waandishi wa habari amesisitiza kwamba Maduro ataachia madaraka kwa makubaliano ama pasipo makubaliano, lakini akisema kwa sasa amejikita katika mabadilishano ya mpangilio na amani.
Machado alizuiwa kugombea katika uchaguzi wa rais mwaka jana, licha ya ushindi mkubwa alioupata kwenye uchaguzi wa awali wa upinzani.