1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Mafuriko mabaya zaidi yaikumba Msumbiji na kusababisha maafa

21 Januari 2026

Watu wasiopunguwa 114 wamefariki na uharibifu mkubwa wa mali umeripotiwa huku baadhi ya vijiji vikifunikwa kabisa na mafuriko yaliyosababishwa na mvua kubwa nchini Msumbiji

Eneo la Kaskazini mwa Msumbiji limewahi kukumbwa na mafuriko mabaya kabisa mnamo mwaka 2007
Eneo la Kaskazini mwa Msumbiji limewahi kukumbwa na mafuriko mabaya kabisa mnamo mwaka 2007Picha: AP

Timu ya waokoaji nchini Msumbiji inaendelea kutafuta watu walionusurika baada ya mafuriko mabaya  kuwahi kuikumba nchi hiyo. Takriban watu 114 wamekufa tangu ulipoanza msimu wa mvua mwanzoni mwa mwezi Oktoba mwaka jana.

Mafuriko mabaya ambayo hayajawahi kuonekana kwa miongo nchini humo,yaliyosababishwa na mvua zinazoendelea kunyesha yameharibu vijiji kadhaa.

Mafuriko yasababisha maafa na uharibifu mkubwa Msumbiji 

Umoja wa Mataifa umesema maji yanayoongezeka yamesababisha hali ya dharura , katika mkoa wa Kusini mwa Maputo timu ya msaada wa dharura imetembelea eneo kubwa lililofunikwa kabisa na maji wakiwatafuta wakaazi waliokwama pamoja na kutathmini uharibifu uliotokea. Msumbiji

Umoja wa Mataifa jana ulisema zaidi ya watu nusu milioni katika nchi hiyo ya wakaazi kiasi milioni 35 wameathirika.

 

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW