1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
PanoramaMsumbiji

Msumbiji yautangaza upya utalii wake

Admin.WagnerD14 Oktoba 2022

Nchini Msumbiji kumefunguliwa maonyesho ya kimataifa ya Utalii kwa lengo la kuiimarisha sekta hiyo, yaliyositishwa kwa akribu miaka miwili kutokana na janga la UVIKO 19.

Mosambik Pemba | Filipe Nyusi
Picha: DW

Rais wa Msumbiji Philipe Nyusi amefungua rasmi Maonyesho ya kimataifa ya utali mjini Maputo yanayokusudiwa kufufua tena sekta hiyo ya utalii ilioshuka kwa asilimia 98 kutokana na mashambulizi ya makundi ya kigaidi pamoja na janga la Uviko 19 liloipiga taifa hilo kwa miaka miwili iliopita. 

Akifungua maonyesho haya ya kimataifa ya utalii rais wa Msumbiji Phillipe Nyusi amesema  Kauli mbiu ya maonyesho haya ni Utalii kama kigezo cha Kuinua Uchumi na ni biashara ya kifahari na kituo cha mikutano kati ya mashirika ya utalii ya kitaifa na taasisi za wenzao kufika hata Australia na sehemu nyengine za ulimwengu. 

"Baadhi ya sehemu za Cabo Delgado zimepoteza utalii kutokana na ugaidi unao tokea huko  lakini sasa tunataka kuwarejesha watalii sehemu hiyo sababu ni sehemu iliokua na vivutio vingi vya utalii." alisema. 

Rais Nyusi amesema majeshi ya nchi rafiki yalioko eneo la Cabo Delgado sasa yameanza kuwarejesha raia wa Msumbiji katika sehemu zao walizozihama.

Soma Zaidi:Wakuu wa SADC walaani uasi nchini Msumbiji 

Mashambulizi ya uasi katika jimbo la Cabo Delgado nchini Msumbiji yalichangia watu wengi kuyakimbia makazi yao.Picha: Delfim Anacleto/DW

Nae waziri wa utalii na utamaduni wa Msumbiji Aldevina Materula  anasema  98% ya utalii wa Msumbiji umeharibika kutokana na vita vya magaidi na tatizo la Uviko19 katika kipindi cha miaka miwili iliopita . 

"Kwa kweli uliharibika sana, hasa tulikua tukikabiliwa na vita viitatu kwa wakati mmoja ukitaja magaidi Kaskazini na pia mkoa wa kati na pia Uviko 19. Na Capo Delgado iko juu juu zaidi katika pembe ya  Kaskazini mwa Msumbiji." 

Waziri Materula anasema masafa yaliopo kutoka Maputo mkoa wa Kati waliopo  hadi kufika Capo Delgado ni sawa na masafa  kutoka Lisbon Ureno hadi Helsinki nchini Iceland kwahivo watu wakilifahamu hilo wataweza kuja Msumbiji kutembelea maeneo mengine mazuri yakuvutia .

Amesema tayari wameshasaini mikataba kadha na mataifa ya jirani kuweza kukuza utalii katika eneo la mataifa ya nchi za kusini mwa Afrika. "Hivi karibuni tulisaini mkataba na Afrika Kusini pamoja na taifa la Eswatini kukuza utalii katika nchi zetu tatu na tena tunaweza  kuwasiliana kwa  Lugha moja. Tunaamini itakua muhimu sana sana sio tu kwa Msumbiji lakini eneo lote la kusini mwa Afrika."

Moja ya tatizo linaloikumba Msumbiji sasa ni deni kubwa serikali ilionalo kuliendesha shirika la ndege la Msumbiji LAM na bado majadiliano yanaendelea kuona iwapo shirika hilo la ndege litabinafshwa kwa wawekezaji 

Maonyesha ya kukuza utalii wa Msumbiji yataendelea hadi siku ya Jumamosi  ijayo.

OMAR  MUTASA  DW  MAPUTO 

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW