1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Mtu mmoja auwawa na mabaki ya droni Urusi

9 Aprili 2026

Mwanamume mmoja ameuliwa na mabaki ya droni iliytunguliwa katika eneo la kusini la Urusi. Ukraine imekuwa ikifanya mashambulizi katika eneo hilo kujibu mashambuli ya Urusi.

Ukraine imekuwa ikifanya mashambulizi kudhibiti uhasama wa Urusi
Ukraine imekuwa ikifanya mashambulizi kudhibiti uhasama wa UrusiPicha: Iryna Rybakova/93rd Separate Mechanized Brigade Kholodnyi Yar/AFP

Mabaki ya ndege isiyo na rubani iliyodunguliwa kusini mwa Krasnodar Krai yamemuua mwanamume mmoja. Hayo ni kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na gavana wa eneo hilo la UrusiVeniamin Kondratyev mapema leo.

Mwanamume huyo aligongwa na mabaki ya ndege isiyo na rubani alipokuwa kwenye roshani ya jengo la ghorofa katika kijiji cha Sauk-Dere katika wilaya ya Krymsk.

Vipande vya ndege zisizo na rubani zilizoharibiwa pia vilianguka kwenye eneo la biashara na katika maeneo kadhaa katika eneo hilo lakini hakuna majeraha yoyote yaliyoripotiwa.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW