Sheria na HakiKenya
Mtuhumiwa kinara wa ujangili Kenya apandishwa kizimbani
17 Septemba 2025
Matangazo
Mwanaume huyo Feisal Mohammed Ali anakabiliwa na mashtaka hayo mapya ikiwa ni miaka tisa tangu alipotiwa hatiani kwa kuhusika na biashara ya pembe na vipusa kabla ya baadae kuachiwa huru.
Yeye na mshtakiwa mwenzake Mohammed Hassan walikamatwa kwenye mji wa mwambao wa Mombasa mwezi uliopita. Walipofikishwa mahakamani jana, wote wawali wameyakana mashtaka ya kuuza nyara za wanyama walio hatarini kutoweka.
Feisal alihukumiwa kifungo cha miaka 20 gerezani mwaka 2016 kwa kusafirisha pembe za ndovu lakini aliachiwa huru kupitia kesi ya rufaa mwaka 2018. Polisi inamtuhumu kuwa nyuma ya mtandao mpana wa ujangili uliosababisha mauaji ya karibu tembo 120.