Museveni: Ushindi unadhihirisha umaarufu wa chama changu
19 Januari 2026
Matangazo
Siku moja baada ya kutangazwa mshindi wa uchaguzi huo, Museveni amesema matokeo hayo yameonyesha uthabiti wa chama chake kinachojulikana kama National Resistance Movement.
"Upinzani ulikuwa na bahati, kwa sababu watu wangu milioni 10 hawakujitokeza. upinzani ungeaibishwa vibaya sana."
Katika hotuba yake hiyo, Museveni pia aliushtumu upinzani kwa kujaribu kuzua vurugu wakati wa upigaji kura.
Amewataka viongozi wa dini kuwashauri vijana ambao huenda wakapotoshwa kuzua vurugu.
Museveni amesema baadhi ya wapinzani wamekosea lakini pia ni magaidi huku akimtaja mpinzani wake wa karibu Bobi Wine na wengine kama wasaliti.