Musharraf atakiwa kuondowa hali ya hatari
17 Novemba 2007Matangazo
John Negraponte naibu waziri wa mambo ya nje wa Marekani wamejadili na Musharraf mzozo wa kisiasa nchini humo na hali nzima ya eneo hilo kutokana na machafuko yanayosababishwa na kundi la Al Qaeda na Taliban.
Wanadiplomasia wa mataifa ya magharibi wanasema Negraponte atamtaka Musharraf kuondowa utawala wa hali ya hatari mara moja,kujiuzulu wadhifa wa ukuu wa majeshi, kuitisha uchaguzi,kuondowa vikwazo dhidi ya vyombo vya habari na kuwaachilia wafungwa wa kisiasa.