1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Musiala alenga kurejea uwanjani tena mwaka 2025

3 Septemba 2025

Kiungo mshambuliaji wa Bayern Munich Jamal Musiala amesema Jumatano kuwa ana imani atarudi tena uwanjani mwaka huu kuichezea hiyo klabu yake.

Jamal Musiala baada ya kuifungia bao Bayern ilipokuwa ikicheza na Dortmund
Jamal Musiala baada ya kuifungia bao Bayern ilipokuwa ikicheza na DortmundPicha: picture alliance / ASSOCIATED PRESS

Hii ni baada ya Musiala kuvunjika mguu na kifundo cha mguu katika Kombe la Dunia la Vilabu huko Marekani mnamo mwezi Julai.

Musiala mwenye umri wa miaka 22, alipata jeraha hilo wakati alipogongana na mlinda lango wa Paris Saint Germain wakati huo Gianluigi Donnarumma.

Musiala alipogongana na Donnarumma na kujeruhiwa vibayaPicha: Rich von Biberstein/Icon Sportswire/IMAGO

"Mguu unaendelea vyema na unapona kulinganana mpango uliowekwa," Musiala aliliambia jarida la SportBild. "Sihitaji magongo ya kutembelea tena ila sitaki kuharakisha mambo. Nitachukua muda unaohitajika."

"Sitaki kuweka tarehe fulani ila kulingana na hatua nilizopiga, nataka kuichezea Bayern tena mwaka huu wa 2025," alisema Musiala.

Hakuna haja ya kumlaumu Donnarumma

Musiala aliyemaliza msimu uliopita akiwa na mabao 21 na kusaidia kuunda mengine 8, Bayern waliposhinda taji la Bundesiga, hajamlaumu Donnarumma kwa jeraha lake akisema majeraha kama hayo hutokea katika kandanda.

"Kisaikolojia, wiki chache za kwnaza hazikuwa rahisi kwangu. Ila hakuna haja ya kuhuzunika kila wakati," alisema Mjerumani huyo.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW