Mwafrika wa Kwanza kuongoza ILO
25 Machi 2022
Mkuu huyo mpya ataanza kazi baadae mwaka huu baada ya mkuu wa sasa Guy Ryder raia wa Uingereza kumaliza muhula wake wa uongozi.
Baada ya duru mbili za upigaji kura, bodi inayoongoza shirika hilo ilimchagua mzee huyo mwenye umri wa miaka 61 kumrithi mwanaharakati wa vyama vya wafanyakazi wa Uingereza Guy Ryder, ambae atatamatisha uongozi wake mwishoni mwa mwezi September baada ya kuhudumu kwa kipindi cha miaka kumi kwenye ofisi hiyo.
Soma zaidi:Shirika la kazi duniani ILO laadhimisha miaka 100
Houngbo ambae kwa hivi sasa ni mkuu wa Mfuko wa Kimataifa wa Maendeleo ya Kilimo wenye makao yake makuu mjini Roma (IFAD), alichaguliwa kutoka miongoni mwa wagombea watano na tangu awali alionekana kuwa na nafasi kubwa ya kushinda uchaguzi huo kutokana na kupata uungwaji mkono mkubwa na wafanyakazi pamoja na Umoja wa Afrika.
Mpambano katika mchakato wa uchaguzi
Wapinzani wake katika kinyang'anyiro hicho walikuwa waziri wa zamani wa kazi wa Ufaransa Muriel Penicaud, waziri wa zamani wa mambo ya nje wa Korea Kusini Kang Kyung-wha, mjasiriamali wa Afrika Kusini Mthunzi Mdwaba, na naibu wa ILO nchini Australia Greg Vines.
Ushindi wa Houngbo unaashiria mabadiliko makubwa kwa ILO, ambayo tangu kuanzishwa kwake mwaka 1919 imekuwa ikiongozwa na wanaume kutoka Ulaya au Amerika pekee.
Soma zaidi:UN: Vifo 745,000 vimetokona na kufanya kazi sana
Shirika hilo kongwe zaidi la Umoja wa Mataifa lina nchi wanachama 187 na wajumbe 56 katika baraza la uongozi huku nusu yao wakiwakilisha serikali, na waliosalia wakiwakilisha waajiri na wafanyakazi.
Hotuba yake ya kwanza baada ya ushindi
Katika hotuba yake ya kwanza baada ya zoezi la upigaji kura na kuibuka na ushindi Houngbo alipongeza mchakato mzima wa uchaguzi. Alisema matokeo ya uchaguzi huo yana ishara nyingi ikiwemo kutimiza matarajio ya kijana wa kiafrika ambaye malezi yake ya unyenyekevu yaligeuka kuwa mafanikio ya haki kwa jamii.
Awali mkuu wa sasa Guy Ryder akizungumza katika baraza lililoongoza uchaguzi huo alimsifu Houngbo kwa kuweka historia na aliona ni heshima kwa mkuu huyo mpya kuliongoza shirika hilo kongwe zaidi la umoja wa mataifa.
soma zaidi:ILO yalenga kuangamiza ajira ya watoto
Houngbo ambae atachukua usukani mnamo Oktoba mosi, atakabiliwa na changamoto kadhaa ikiwemo marekebisho ya kanuni za shirika hilo zinazoshughulikia masuala ya ajira ulimwenguni katika kipindihichi ambacho mabadiliko ya teknolojiwa yanashuhuduwa kwa kasi.