Mwaka mpya 2012 utakuwa wa matatizo; Merkel
1 Januari 2012Katika hotuba yake kansela alianzia kwa kuangalia masuala ya kimataifa. Amesema kuwa mwanzoni mwa mwaka huu lilianza vuguvugu la mageuzi ya kisiasa katika mataifa ya Afrika kaskazini na mashariki ya kati. Mwezi March Japan ilikumbwa na tetemeko kubwa la ardhi , na kusababisha maafa makubwa ya kinyuklia. na katika majira ya mapukutiko mwishoni mwa mwaka huu mkaazi wa bilioni saba alizaliwa katika jumla ya wakaazi duniani.
Ameongeza kuwa ulikuwa mwaka wenye mabadiliko makubwa. Hayo pia yalitokea katika bara la Ulaya.
Katika bara la Ulaya hali iliendelea kuwa mbaya ya madeni ya nchi, amesema kansela, na kuongeza kuwa mbali ya matatizo yote hayo hatukusahau, kwamba kuishi kwa usalama ni zawadi ya kihistoria kwa bara hili. Kwa muda wa nusu karne kumekuwa na uhuru , amani , sheria , haki za binadamu na demokrasia.
Maadili haya tusingeweza pia katika enzi hizi kuyalinda vizuri. Kwa hivi sasa , ambapo bara la Ulaya linajikuta katika wakati mgumu kabisa kuwahi kutokea kwa karne kadha, natambua kuwa mnafikiria kuhusu usalama wa sarafu yetu. Amesema kuwa bara la Ulaya linapambana na mzozo huu kwa pamoja , licha ya kuwa njia kuelekea kuudhibiti mzozo huo ni ndefu na itakuwa na matatizo.
Kuhusu hali ya hapa Ujerumani kansela amesema :
Hapa Ujerumani tuna sababu ya kuwa na matumaini. Kwani karibu kila kijana wetu amepata nafasi ya masomo katika mwaka huu. Ni watu wachache wasio na ajira. Ujerumani imo katika njia iliyo sahihi, licha ya kuwa mwakani bila shaka kutakuwa na hali ngumu.
Hiyo ni sehemu ya hotuba ya kansela Angela Merkel ya kuukaribisha mwaka mpya 2012.