1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Mwanajeshi mmoja na wanamgambo wanne wauwawa Kongo

12 Mei 2023

Mwanajeshi mmoja na wanamgambo wanne wameuwawa katika shambulizi karibu na mji mkuu wa Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo, Kinshasa, katika wimbi la hivi karibuni la machafuko magharibi mwa nchi hiyo.

DR Kongo | kongolesische Soldaten auf dem Weg zur Front im Kampf gegen die M23-Rebellen
Picha: Arlette Bashizi/AFP/Getty Images

Taarifa hizo ni kwa mujibu wa jeshi la Kongo ambalo limesema kundi la wapiganaji linalofahamika kama "Mobondo" ndiyo limehusika na shambulizi hilo. Msemaji wa jeshi la Kongo Sylvain Ekenge amesema kundi hilo lilikivamia kijiji cha Nguma Alfajiri ya jana Alhamisi na katika mapambano yalitokea mwanajeshi mmoja alipoteza maisha kutokana na majeraha.

Soma zaidi:DRC: Mauaji dhidi ya raia yanaendelea licha ya uwepo wa vikosi vya usalama

Kundi la Mobondo linahusishwa na jamii iitwayo Yaka ambayo imo kwenye mzozo wa kuwania hatimiliki za ardhi na kabila lingine la Teke. Mapigano kati ya jamii hizo yamekuwa yakiripotiwa zaidi kwenye jimbo la Mai-Ndombe na ikadiriwa zaidi ya watu 300 wameuwawa tangu mwezi Juni mwaka jana.

 

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW