1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Mpinzani wa Tunisia aliye gerezani asitisha mgomo wa kula

2 Desemba 2025

Mwanasiasa wa upinzani nchini Tunisia, Jawhar Ben Mbarek, aliyehukumiwa kifungo cha miaka 20 jela kwa madai ya kushiriki njama dhidi ya serikali, amesema amesitisha mgomo wa kula aliokuwa akiendesha kwa mwezi mmoja.

Tunisia Tunis 2023 | Waislamu wa madhehebu ya Shia nchini Tunisia
Rais Kais Saied Tunis, Tunisia. Tarehe: 4 Mei 2023.Picha: Tarek Guizani/DW

Katika ujumbe kwenye mitandao ya kijamii  uliochapishwa na dada yake, wakili Dalila Mssadek, mwanasiasa huyo mwenye umri wa miaka 57 ameandika matukio mawili ya maandamano ya  hivi karibuni ya mashirika ya kiraia yamedhihirisha kuwa "barabara ya kidemokrasia iliyo hai” inatetea haki za wafungwa wa kisiasa, na hivyo anaweza kusitisha mgomo wake wa siku 33. Ben Mbarek, mwanzilishi mwenza wa muungano wa upinzani wa Tunisia uitwao National Salvation Front (FSN), alikuwa miongoni mwa washtakiwa takriban 40, wengi wao wakosoaji wa Rais Kais Saied, waliotiwa jela Ijumaa kwa ‘njama dhidi ya usalama wa taifa'.Umoja wa Mataifa na mashirika ya haki za binadamu yamekosoa kesi hiyo, na mashtaka yalijikita zaidi katika madai ya kukutana na wanadiplomasia wa kigeni. Washtakiwa walihukumiwa mwezi Aprili na wiki iliyopita wakapewa vifungo vya hadi miaka 45.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW