1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Mwili wa Odinga kuagwa kitaifa mjini Nairobi

17 Oktoba 2025

Mwili wa kiongozi mkongwe wa upinzani nchini Kenya Raila Odinga utaagwa kitaifa leo Ijumaa kwa ibada maalamu mjini Nairobi na kuhudhuhuriwa na viongozi wakuu na wawakilishi wa serikali mbalimbali duniani.

Mwili wa Raila Odinga ulipowasili nchini Kenya siku ya Alhamisi ukitokea India
Mwili wa Raila Odinga ulipowasili nchini Kenya siku ya Alhamisi ukitokea India.Picha: Andrew Kasuku/AP Photo/picture alliance

Vyombo vya habari nchini Kenya vimeripoti kuwa ibada hiyo itafanyika kwenye uwanja wa michezo wa Nyayo na kuongozwa na Rais William Ruto wa nchi hiyo.

Odinga, mwanasiasa kigogo wa upinzani aliaga dunia siku ya Jumatano akiwa nchini India alikokwenda kwa matibabu.

Mwili wake ulirejeshwa nyumbani jana Alhamisi na maelfu ya watu walipata nafasi ya kutoa heshima za mwisho kwenye uwanja wa Kasarani nje kidogo ya mji mkuu Nairobi.

Hata hivyo zoezi hilo lilikumbwa na vurumai iliyosababisha vifo vya watu wasiopungua watatu ya baada ya polisi kufyetua risasiili  kuwatawanya waombolezaji waliokuwa wakisongamana kuelekea jukwaa la watu mashuhuri.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW