1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Mwili wa Odinga wawasili Kisumu tayari kuagwa na umati

18 Oktoba 2025

Umati mkubwa wa waombolezaji umekusanyika leo Jumamosi katika mji wa magharibi mwa Kenya, Kisumu ili kuaga mwili wa mwanasiasa mkongwe Raila Odinga

Kenya Nairobi 2025 | Vikosi vya usalama vikijaribu kudhibiti umati wa watu kwenye mazishi ya Odinga
Vikosi vya usalama vikijaribu kudhibiti umati wa watu kwenye mazishi ya OdingaPicha: Tony Karumba/AFP/Getty Images

Umati mkubwa wa waombolezaji umekusanyika leo Jumamosi katika mji wa magharibi mwa Kenya, Kisumu ili kuaga mwili wa mwanasiasa mkongwe Raila Odinga. Maombolezo ya Odinga aliyefariki dunia Jumatano wiki hii, yamegubikwa na ghasia na kusababisha vifo vya watu watano mjini Nairobi kutokana na umati mkubwa wa watu uliojitokeza kumuaga.

Kulikuwa na dalili za kutokea ghasia tena wakati jeneza la mwili wake lilipokaribia uwanja wa Kisumu, huku kundi kubwa la waombolezaji likikiuka vizuizi vya usalama na kupanda kwenye kuta.

Vikosi vya usalama vililazimika kufyatua risasi siku ya Alhamis, ili kutawanya umati mkubwa katika uwanja wa michezo jijini Nairobi ambako mwili wa Odinga ulipelekwa kuagwa. Maombi ya kitaifa yalifanyika jana Ijumaa na kuongozwa na Rais wa Kenya William Ruto. Odinga atazikwa kesho Jumapili katika eneo la Bondo karibu na kaunti ya Siaya.

 

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW