NAIROBI: Washukiwa sita wauwawa kwa kupigwa risasi
28 Mei 2007Polisi nchini Kenya wamesema watu sita walioshukiwa kuwa majambazi waliuwawa kwa kupigwa risasi wakati maafisa wa polisi walipokabiliana nao mjini Nairobi Kenya.
Mtoto wa umri wa miaka 10, mwanamume mmoja mzee, maafisa wawili wa polisi na washukiwa wawili walikufa katika mapambano hayo ya risasi.
Mapambano hayo yaliyotokea baada ya maafisa watatu wa polisi kuwatia mbaroni watu wawili walioshukiwa kuwa majambazi wakati walipokuwa wakishika doria kwenye mtaa wa mabanda wa Kariobangi kaskazini mashariki mwa jiji la Nairobi.
Kamanda wa polisi wa eneo hilo, Paul Ruto, amesema hakuna aliyekamatwa katika kisa hicho na hawezi kuthibitisha ikiwa washukiwa hao ni wanachama wa kundi la Mungiki ambalo limekuwa likiwahangaisha Wakenya katika siku chache zilizopita.