1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaKosovo

NATO kutuma wanajeshi 700 zaidi Kosovo, kukabili maandamano

31 Mei 2023

Jumuiya ya kujihami ya NATO imetangaza kuwa itatuma wanajeshi 700 zaidi kaskazini mwa Kosovo ili kusaidia kuzima maandamano yenye vurugu kufuatia makabiliana kati ya Waserbia na vikosi vya kulinda amani.

Wanajeshi wa vikosi vya kulinda usalama vya KFOR wakionekana kulilinda jengo la manispaa lililo katika mji wa Zvecan, Kosovo lililozingirwa na waandamanaji.
Marekani na Umoja wa Ulaya zimeongeza juhudi za upatanishi kati ya Serbia na Kosovo kwa hofu ya kuongezeka mzozo.Picha: Ognen Teofilovski/REUTERS

Tayari walinda amani 30 wamejeruhiwa katika vurugu hizo. Vurugu hizo zilitokea kuanzia wiki iliyopita baada ya mameya wa kabila la Albania waliochaguliwa katika uchaguzi wa serikali za mitaa uliosusiwa na Waserbia, walipojaribu kuingia ofisini. Wakati Waserbia walipowazuia, polisi ya Kosovo ilirusha mabomu ya machozi ili kuwatawanya waandamanaji. Marekani na Umoja wa Ulaya zimeongeza juhudi zao za upatanishi kati ya Serbia na Kosovo wakihofia kukosekana kwa utulivu katika eneo hilo hasa wakati huu ambapo vita vingali vinaendelea nchini Ukraine.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW