1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaUbelgiji

NATO yaapa kuiunga mkono Ukraine bila kuchoka

24 Februari 2023

Jumuiya ya Kujihami ya NATO imetangaza leo Ijumaa kwamba imedhamiria katika kuiunga mkono Ukraine na kusema jitihada za Urusi katika kuvunja azimio la watu jasiri wa Ukraine zinashindwa.

Belgien | NATO | Treffen Jens Stoltenberg mit Dmytro Kuleba und Josep Borrell
Picha: Valeria Mongelli/AFP/Getty Images

Katika taarifa yake iliyoitoa ikiwa ni mwaka mmoja baada ya uvamizi wa Urusi nchini Ukraine, NATO imesema Urusi inapaswa kusitisha vita vyake haramu, ambavyo vinaathiri utaratibu wa usambazaji wa chakula na nishati ulimwenguni na kuitaka Moscow kuwajibika kutokana na uhalifu wake wa kivita.

Kadhalika tamko hilo pia limewajumuisha wanaoiwezesha Urusi katika vita hivyo vilivyogharimu maisha ya maelfu ya raia, wengine wakikimbia taifa hilo, ikiwa ni pamoja na Belarus na Iran ambayo iliipatia Urusi ndege zisizokuwa na rubani aina ya Shaheed.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW