1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Navalny alikuwa abadilishwe na mfungwa wa Kirusi Ujerumani

26 Februari 2024

Washirika wa kiongozi wa upinzani wa Urusi aliyefariki akiwa kifungoni, Alexei Navalny, wamesema kiongozi huyo alifariki dunia wakati mazungumzo ya kumbadilisha na mfungwa mmoja wa Urusi nchini Ujerumani.

Mashada ya mauwa yakiwekwa mbele ya picha ya Alexei Navalny mjini Helsinki, Finland.
Mashada ya mauwa yakiwekwa mbele ya picha ya Alexei Navalny mjini Helsinki, Finland. Picha: LEHTIKUVA/REUTERS

Washirika hao walisema muda mfupi kabla ya kifo chake, mazungumzo yalikuwa yako njiani ili kubadilishana naye na mfungwa wa Urusi aliyefungwa nchini Ujerumani, Vadim Krasikov..

Katika taarifa aliyotoa kwa njia ya vidio, Maria Pevchikh - mshirika wa Navalny anayeishi nje ya Urusi - alisema alipokea uthibitisho kwamba mazungumzo hayo yalikuwa katika awamu ya mwisho mnamo Februari 15, siku moja kabla ya Navalny kuripotiwa kufa.

Kulingana na Pevchikh, Navalny na raia wawili wa Marekani waliokuwa wamefungwa nchini Urusi walikuwa sehemu ya makubaliano hayo ya kubadilishana wafungwa. 

Krasikov alikuwa anatumikia kifungo cha maisha jela nchini Ujerumani kwa mauaji ya mwaka 2019 mjini Berlin ya  Zelimkhan "Tornike" Khangoshvili, raia wa Georgia mwenye asili ya Chechen.

Hata hivyo, majina ya raia wa Marekani hayakutajwa.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW