1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Navalny kuzikwa Moscow

1 Machi 2024

Kiongozi wa upinzani nchini Urusi, Alexei Navaly, aliyeaga dunia gerezani wiki mbili zilizopita, alitarajiwa kuzikwa siku ya Ijumaa kwenye mji mkuu wa nchi hiyo, Moscow.

Waombolezaji wakiwa na picha ya marehemu Alexei Navalny
Waombolezaji wakiwa na picha ya marehemu Alexei Navalny.Picha: Dawid Zuchowicz/Agencja Wyborcza.pl/REUTERS

Ilitarajiwa kungekuwepo idadi kubwa ya polisi wakati wa mazishi hayo yaliyofanyika mchana wa Ijumaa katika makaburi ya Borisov baada ya ibada kanisani.

Kulikuwa na hofu kwamba maafisa wa polisi wangeliwazuia baadhi ya waombolezaji.

Soma zaidi: Navalny atarajiwa kuzikwa kusini mwa jiji la Moscow

Hivi karibuni mamia ya watu walikamatwa na polisi kwa kuweka mashada ya maua kumuomboleza Navalny.

Kulingana na taarifa rasmi ya serikali, Navalny aliyekuwa na umri wa miaka 47, na pia mkosoaji mkubwa wa Rais Vladimir Putin, alikufa Februari 16 akiwa gerezani.

Mjane wake, Yulia Navalnaya, na timu yake ya wanaharakati, walimtuhumu Rais Putin kwa kumuua mwanasiasa huyo.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW