1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Nchi za EU zakubaliana kuiwekea Urusi vikwazo vipya

20 Juni 2024

Nchi wanachama za Umoja wa Ulaya zimekubaliana kuiwekea Urusi vikwazo vipya, vinavyolenga kwa kiasi kikubwa kukabiliana na mianya inayokwepa vikwazo vilivyowekwa hadi sasa.

Makao makuu ya Umoja wa Ulaya Brussels
Tangu Urusi ianzishe vita kamili Ukraine, Umoja wa Ulaya umeweka vikwazo kulenga uchumi na maafisa wa UrusiPicha: Cornelius Poppe/NTB/picture alliance

Hayo yameelezwa na Ubelgiji ambayo ni rais zamu wa Umoja wa Ulaya. Tangu Urusi ianzishe vita kamili nchini Ukraine, Umoja wa Ulaya umeweka vikwazo kulenga uchumi, taasisi na maafisa wa Urusi. Hata hivyo, Urusi imejitahidi kutafuta njia ya kuvikwepa vikwazo hivyo ili kuweza kuendesha uchumi na shughuli zake za kijeshi.

Soma pia: Putin: Urusi inasalia kuwa mshirika mkubwa wa kibiashara duniani licha ya vikwazo

Lengo la hatua zinazochukuliwa na Umoja wa Ulaya ni kuizuia Urusi kupata teknolojia ya nchi za Magharibi, inayoweza kutumiwa kwa madhumuni ya kijeshi.

Kansela wa Ujerumani Olaf Scholz amekiri kwamba nchi yake ina wasiwasi huenda vikwazo hivyo vikaziathiri kampuni za Ujerumani zinazouza bidhaa nje ya nchi.

 

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW