1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Nchi za EU zatakiwa kuionyesha Ukraine kuwa zinaiunga mkono

19 Machi 2026

Mkuu wa sera za kigeni wa Umoja wa Ulaya Kaja Kallas, amesema sasa ni wakati wa dharura wa Jumuiya hiyo kuonyesha uungaji wake mkono katika juhudi za Ukraine kwenye vita vyake na Urusi.

Belgien Brüssel 2026 | EU-Außen- & Energieministertreffen | Kaja Kallas bei Pressekonferenz
Picha: Omar Havana/REUTERS

Mkuu huyo wa sera za kigeni wa Umoja wa Ulaya, amesema Jumuiya hiyo inapaswa kuionyesha Ukraine uungaji wake mkono wakati ambapo Rais wa Hungary Viktor Orban anapoendelea kuzuia mkopo unaohitajika sana na serikali ya Kiyv kutokana na nchi hizo mbili kuwa kwenye mvutano.

Kallas aliwaambia waandishi wa habari alipowasili katika eneo la mkutano wa kilele wa viongozi wa Umoja wa Ulaya mjini Brussels ambako viongozi hao wanatarajia kuidhinsiha ufadhili wa euro bilioni 90 ambazo Hungary ilisaini mwezi Desemba pamoja na nchi nyingine wanachama wa Umoja wa Ulaya.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW