1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Ndege za Israel zashambulia kusini mwa Lebanon

Josephat Charo
20 Machi 2026

Israel imefanya mashambulio mapya katika maeneo ya kusini mwa Lebanon. Watu kadhaa wanaripoti kujeruhiwa katika hujuma hizo.

Israel imeyashambulia maeneo ya kusini mwa Lebanon ukiwemo mji wa Tyre.
Israel imeyashambulia maeneo ya kusini mwa Lebanon ukiwemo mji wa Tyre.Picha: Kawnat Haju/AFP

Israeli ilifanya mashambulizi katika miji iliyo kusini mwa Lebanon, na kusababisha watu wengi kujeruhiwa. Hayo yameripotiwa na vyombo vya habari vya serikali Ijumaa.

Shirika rasmi la habari la kitaifa la Lebanon limeripoti kamba ndege za kivita za adui Israeli zilishambulia alfajiri, zikiilenga miji ya Bafliyeh na Hanine katika wilaya za Tyre na Bint Jbeil na kuongeza kuwa vikosi vya Israel vilikuwa vimeishambulia miji mingine mitano kusini mwa nchi.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW