1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaChina

Ndege za kivita za China zaingia eneo la kijeshi la Taiwan

Daniel Gakuba
8 Juni 2023

Wizara ya ulinzi ya Taiwan imesema kuwa ndege za kijeshi za China zaidi ya 30 zimeingia katika eneo la Taiwan la ulinzi wa anga, lakini bila kufika katika anga la mipaka ya kisiwa hicho.

Ndege za kijeshi za China zikiwa zinafanya majaribio ya kujaza mafuta angani.
China na Taiwan zimekuwa katika mvutano wa kila wakati kutoana na madai ya China ya kukidhibiti kisiwa hicho.Picha: CCTV/AP/picture alliance

Msemaji wa wizara ya ulinzi mjini Taipei Sun Li-Fang amesema ndege za China zimeanza kuingia katika eneo la ulinzi la Taiwan saa kumi na moja alfajir, na kwamba zoezi hilo limehusisha ndege 37. Msemaji huyo ameongeza kuwa baadhi ya ndege hizo zimeendelea hadi magharibi mwa bahari ya Pasifiki kuendelea na luteka za upelelezi.

Wizara  ya ulinzi ya kisiwa hicho ambacho China inadai ni himaya yake, imesema imeendelea kuifuatilia kwa makini hali hiyo, na kwamba iliweka tayari meli na ndege zake na kuyaweka makombora katika hali ya tahadhari.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW