1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW
SiasaIsrael

Netanyahu aenda Marekani kuujadili mpango wa nyuklia wa Iran

10 Februari 2026

Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu anaelekea Marekani hii leo ambapo watajadiliana na Rais Donald Trump kuhusu mazungumzo ya nyuklia ya Iran.

Marekani Palm Beach 2025 | Donald Trump na Benjamin Netanyahu kwenye mkutano na waandishi wa habari
Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu amekwenda marekani kuzungumza na Rais Donald Trump kuhusu mpango wa nyuklia wa Iran Picha: Jim Watson/AFP

Israel inashinikiza makubaliano hayo yajumuishe Iran kusitisha urutubishwaji wa aina yoyote wa madini ya urani, kupunguza mipango yake ya makombora na kuacha kuwasaidia makundi ya wanamgambo kama ya Hamas na Hezbollah.

Lakini Iran inayapinga masharti hayo na kusema itakubaliana tu na kiwango fulani cha ukomo kwenye mpango wa nyuklia ili badala yake iondolewe vikwazo vya kiuchumi.

Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje wa Iran Esmail Baqaei mapema leo ameilaumu Israel kwa kupinga kila mchakato wa kidiplomasia unaolenga kuleta amani ya kikanda.

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW