1. Nenda kwenye maudhui
  2. Nenda kwenye orodha kuu
  3. Nenda tovuti zaidi za DW

Netanyahu yupo Marekani kujadili usitishaji vita Gaza

7 Julai 2025

Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu amewasili Marekani kwa ziara ya siku kadhaa, wakati juhudi za usitishaji mapigano zikiendelezwa ili kumaliza vita vya miezi 21 katika Ukanda wa Gaza.

Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu
Netanyahu amewasili Marekani kujadili mpango wa usitishaji vita Gaza Picha: Menahem Kahana/AFP

Hii ni ziara ya Tatu ya Netanyahu nchini humo tangu Rais wa nchi hiyo Donald Trump alipoingia madarakani miezi sita iliyopita. 

Donald Trump amewaambia waandishi habari mjini New Jersey kwamba, anaamini mpango wa kusitisha mapigano na hatua ya kuwaachia mateka wanaoshikiliwa na wanamgambo wa Hamas huenda ukafikiwa wiki hii.

Wapalestina zaidi ya 30 wauawa Ukanda wa Gaza

Ziara ya Netanyahu nchini Marekani inafanyika chini ya wiki mbili baada ya kumalizika vita vilivyodumu kwa siku 12 kati ya Israel na Jamhuri ya Kiislamu ya Iran ambako mashambulizi ya Israel na Marekani yaliharibu kinu muhimu cha nyuklia cha Iran. 

Netanyahu amesema mashambulizi hayo yaliyosababisha vifo vya zaidi ya watu 900 kulingana na maafisa wa Iran yatawezesha kutanua juhudi za amani kuliko ilivyokuwa zamani. 

Ruka sehemu inayofuata Taarifa kuu ya DW

Taarifa kuu ya DW

Ruka sehemu inayofuata Taarifa zaidi kutoka DW